HALMASHAURI
YA JIJI LA DAR ES SALAAM
TANGAZO
LA NAFASI YA KAZI YA KUKUSANYA USHURU WA MAEGESHO KATIKA MANISPAA YA TEMEKE NA
KIGAMBONI.
Mkurugenzi wa
Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam anawatangazia wakazi wa Dar es Salaam
wenye sifa, nafasi ya kazi ya kukusanya mapato ya maegesho katika Manispaa ya Temeke na Kigamboni jumla ya
Nafasi Sitini (60). Kazi hii itakuwa ni ya Mkataba wa miezi mitatu na mshahara
utalipwa kwa kuzingatia Sheria ya Ajira Cap. 300 “Wage Order” 2013 ambao
utakuwa sh.150,000/= kwa mwezi.
SIFA
ZA MWOMBAJI:
·
Awe Raia wa Tanzania mwenye umri
usiopungua miaka 18 na umri usiozidi miaka 60
·
Awe na elimu ya darasa la Saba na
kuendelea
·
Awe na uwezo wa kutumia “Smart phone”
katika miamala ya malipo
·
Awe na Uzoefu usiopungua miezi sita katika
masuala ya kukusanya Ushuru.
·
Awe mwadilifu na mwaminifu na awe
hajawahi kutiwa hatiani kwa kosa la jinai
MAELEKEZO
YA JUMLA
·
Waombaji waambatishe vivuli vya vyeti
vya taaluma zao pamoja na cheti cha kuzaliwa
·
Kila barua ya muombaji iambatishwe na
picha moja ndogo (Passport size) iliyopigwa siku za karibuni.
·
Barua ya Maombi iambatishwe na:
-
Barua kutoka kwa wadhamini wawili ambao
ni watumishi wa Serikali zikiwa na picha “Pass port size” ya hivi karibuni, Anuani
kamili ya makazi, pamoja na namba zao za
simu.- Barua ya Utambulisho kutoka kwa Mwenyekiti wa Serikali za Mitaa.
- Wasifu (CV)
·
Waombaji watakaokuwa “Shortlisted”
watajulishwa kwa njia ya simu tarehe ya usaili.
·
Barua ya maombi ya kazi iletwe kwa njia
ya mkono katika Ofisi ya Mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam kuanzia tarehe ya
tangazo hili au kwa njia ya posta kupitia anuani tajwa hapo chini kuanzia saa mbili
kamili (2:00) asubuhi hadi saa 8:00 mchana.
Mwisho wa kupokea maombi ya kazi ni tarehe 27 Disemba, 2016 saa 8:00 mchana.
Maombi yatumwe kwa
Anuani ifuatayo:-
Mkurugenzi wa Jiji,Halmashauri ya Jiji,
Ukumbi wa Jiji,
1 Barabara ya Morogoro,
S.L.P. 9084,
11882 – DAR ES SALAAM
Tangazo hili pia linapatikana kwenye tovuti ya Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam ambayo ni www.dcc.go.tz
Sipora J.Liana
MKURUGENZI WA
JIJI
HALMASHAURI YA JIJI LA
DAR-ES-SALAAM
v
0 comments:
POST A COMMENT