
Wanawake
 wa kijiji cha Kisungamile kilichopo katika Kata ya Matai wilayani 
Kalambo katika mkoa wa Rukwa wamemwadhibu Vitus Nyami (26) kwa 
kumtembeza nusu uchi na kulazimisha kula kinyesi cha ng’ombe kwa kosa la
 kumtukana mama yake mzazi matusi ya nguoni.
Aidha
 wanawake hao walitumia mfuko wa ‘salphate’ kufunika sehemu za siri za 
kijana huyo kisha wakaanza kumtembeza mitaani kijijini  humo huku 
wakiimba nyimbo za kabila la Kifipa wakilaani tabia ya kijana huyo ya 
kumtukana mama yake mzazi matusi ya nguoni kila kukicha .
Walidai
 kukasirishwa na tabia ya kijana huyo wa kiume kumtukana mzazi wake wa 
kike matusi ya nguoni, hivyo walilazimika kumfunga kamba na kumtembeza 
mitaani kijijini humo akiwa nusu uchi.
Mwenyekiti
 wa kijiji cha Kisungamile, Didas Musa alikiri kutokea kwa mkasa huo 
juzi ambapo mtuhumiwa huyo alitembezwa mitaani kwa saa sita kuanzia saa 
1:00 asubuhi hadi saa 6:00 mchana.
Akifafanua
 alisema kuwa licha ya adhabu hiyo ya kutembezwa nusu uchi mitaani na 
kucharazwa viboko 15, pia ameamriwa kulipa mbuzi mmoja, unga wa sembe 
debe moja na mafuta ya kupikia lita moja.
“Adhabu hii kwa kijana hutolewa na akina mama ambapo mimi kama kiongozi kazi yangu ni kuibariki tu,”
 alisisitiza . Mkazi wa kijiji hicho, Obedi Mwanakatwe alisema kijana 
huyo amekuwa akimtukana mama yake mara kwa mara , tabia ambayo imekuwa 
ikiwachukiza akinamama kijijini humo ambapo waliandamana na kumkamata 
kijana huyo .
“Baada
 ya akinamama hao wenye hasiri kumkamata kijana huyo walimpeleka kwenye 
shimo lililojaa kinyesi cha ng’ombe kisha wakampaka kinyesi hicho mwili 
mzima wakiwa wamechanganya na unga wakisaidiwa na wanaume, walimtembeza 
uchi kijana huyo mitaani kijijini humo,” alieleza.
Stela
 Tenganamba alisema baada ya kumtembeza kwa muda mrefu waliamua kumlisha
 kinyesi cha ng’ombe na kumpaka mwili mzima sambamba na kumroweka kwenye
 matope.
Adhabu
 hiyo iliwekwa enzi za mababu zao , ambapo mtu yeyote anayetukana matusi
 hadharani huchukuliwa hatua hiyo sambamba na kulipishwa ng’ombe mmoja, 
mbuzi, unga debe moja na mafuta ya kupikia lita moja.
Akifafanua
 alisema kuwa baada ya kutembezwa mitaani akiwa uchi hupelekwa kwa 
Mwenyekiti wa Kijiji ambaye hutoa adhabu kulingana na akinamama 
watavyoona inafaa
                                picha na Gaspal simon mazengo
                                      maswayetu term 
                    ahsante kwa kutembelea blog yetu 
v
 
 
 

0 comments:
POST A COMMENT