 
 
Mauaji
 ya kutumia silaha za moto yameendelea kushamiri nchini,baada ya 
mfanyabiashara mmoja mjini Singida kufariki dunia baada ya kupigwa 
risasi ya bunduki aina ya bastola wakati akitaka kuondoka dukani kurejea
 nyumbani.
Mfanyabiashara huyo na mkazi wa Itungukia tarafa ya Mungumaji manispaa Singida ni Simon Charles (49).
Akizungumza
 na waandishi wa habari ofisini kwake Kamanda wa jeshai la polisi mkoa 
wa Singida,ACP Debora Magiligimba, alisema tukio hilo la kusikitisha 
limetokea Aprili, 20 mwaka huu saa 3.30 usiku.
Alisema
 siku ya tukio baada ya mfanyabiashara huyo kufunga duka lake la madawa 
ya binadamu lililopo standi ya zamani ya mabasi alianza kuelekea kwenye 
gari lake ili aweze kurejea nyumbani kwake.
“Wakati
 akikaribia gari lake ghafla muuaji huyo ambaye alijificha upande 
mwingine wa gari hilo alinyanyuka na kumpiga risasi titi la upande wa 
kulia na kutokea nyuma na kisha kudondoka pale pale. Wasamaria wema 
waliweza kumkimbiza hospitali ya mkoa lakini alifariki akipatiwa 
matibabu.Kifo chake kinatokana na kuvuja damu nyingi,” alisema Magiligimba. 
Kamanda
 huyo alisema kwenye eneo la tukio kulipatikana ganda moja la risasi ya 
bastola. Hadi sasa chanzo cha mauaji hayo, bado hakijajulikana.
Katika
 hatua nyingine, Magiligimba alisema kuwa Jeshi la Polisi linaendelea na
 msako mkali kubaini watu waliojihusisha na tukio hilo ili waweze 
kukamatwa na sheria ziweze kuchukua mkondo wake.
“Jeshi
 la polisi linatoa wito kwa wananchi wote mkoani kutoa ushirikiano kwa 
jeshi hilo ili kusaidia kukamatwa kwa wauaji hao. Pia wafanyabiashara 
tunawakumbusha umuhimu wa kuajiri walinzi, watakaowalinda wao na mali 
zao,” alisisitiza.
Habari
 kutoka eneo la tukio, zinaeleza kwamba mfanyabiashara huyo ambaye 
kitaaluma ni daktari wa binadamu ameauwa na mtu mmoja ambaye alivalia 
suruali. Baada ya mauaji hayo, mtu huyo aliondoka kwa miguu na kutokomea
 kusiko julikana.
Mashuhuda
 wengine wanadai kuwa muuaji huyo hakuweza kukamatwa wala kufukuzwa, kwa
 madai kuwa mlio wa risasi ya bastola haukuwa mkubwa hivyo wakahisi kuwa
 ni tairi la pikipiki limepasuka na hivyo walipuuzia.
          picha na Gaspal simon mazengo
           maswayetu term 2017 
v
 
 
 

0 comments:
POST A COMMENT